BREAKING NEWS, HAYA HAPA MATOKEO YA DARASA LA SABA 2019




Matokeo ya darasa la saba 2019, yametangazwa. NECTA imeeleza ufaulu umeongezeka kwa asilimia 3.78. Waliofaulu ni asilimia 81.50 ya watahiniwa 933,369. Pia Watahiniwa 909 wamefutiwa matokeo kwa sababu mbalimbali ikiwemo udanganyifu.


Katibu Mtendaji wa NECTA Dkt Charles Msonde
amesema mwanafunzi aliyeongoza Kitaifa ni Grace Manga kutoka Shule ya Msingi Graiyaki Mara, akifuatiwa na Francis Gwagi kutoka Shule ya Msingi Paradise ya Geita.


Amesema kuwa aliyeshika nafasi ya tatu ni Loi Kitundu kutoka Shule ya Msingi Mbezi ya Dar es Salaam, na Victor Godfrey kutoka Graiyaki ameshika nafasi ya nne.
"Katika ufaulu wa masomo, somo la Kiswahili, Kiingereza na Sayansi katika mtihani huo ufaulu wake umepanda na somo la Hisabati umeshuka,"

This is received, thanks for your comments, will come back to you

Previous Post Next Post