Jiji la Arusha lawapa Walimu zaidi ya 200, motisha ya Mil81

 Na Mwandishi Wetu,Arusha

Halmashauri ya Jiji  la Arusha imetoa kiasi cha Milioni 81 kwa ajili ya kuwapa motisha walimu zaidi ya 200 ambao walifaulisha masomo yao kwa kipindi cha mwaka 2020 2021 ,pamoja na wanafunzi ambao walifanya vema 


 Akikabidhi fedha pamoja na zawadi kwa walimu hao mapema jana kwenye viwanja vya Ngarenaro mkurugenzi wa jiji la Arusha, Dkt Pima alisema kuwa wameamua kutoa motisha ili kuendelea kufuta ziro.



Alisema kuwa fedha hizo zina baraka ya baraza la madiwani na wao pia wame bariki kufanyika kwa zoezi hilo ambapo wamedai ni  moja ya njia ya kuipandisha halmashauri kiufaulu


"Tuna walimu zaidi ya 200 hapa na hawa walimu wanaopata zawadi leo ni wale wa shule  za sekondari,msingi,shule binafsi kwa upande wa msingi lakini na wanafunzi bora 


Hawa walimu wamegaeanyika katika makundi makundi kuna ambao shule zao zilifanikiwa kufuta ziro kabisa ,kuna nyingine ambazo miaka ya nyuma zilikuwa zinaongoza kwa kuwa wamwisho ila sasa wamejitaidi na wametoka huko hivyo basi tumewapongeza kwa njia hiyo"aliongeza Dkt Pima 


Aliwataka walimu ambao hawakuguswa na zoezi hilo la utoaji wa fedha pamoja na zawadi kuhakikisha kuwa wanafundisha kwa bidii sana masomo yao na kupata ufaulu wa daraja la juu ili waweze kupata zawadi na motisha kama hiyo kwa kipindi kijacho 



Awali mkuu wa mkoa wa Arusha, John Mongela alisema kuwa ualimu ni kazi nzuri sana na inatakiwa kueshimiwa sana ikiwa ni pamoja na kubuni namna ya kuendelea kuwapa motisha 


Mongela alisema unapomuona kiongozi ambaye yupo imara basi jua ya kuwa mwalimu wake wa ngazi za chini alimsimamia vema katika ukuaji wake 


"Nataka tu niwambie kuwa taifa hili linawategemea sana ninyi walimu hasa kwenye malezi na ukuaji wa watoto wetu nawapongeza sana Jiji kwa kubuni jambo hili ambalo limekuwa ni motisha nzuri"alisema


Aliwataka walimu hao kuendelea kuhubiri amani kwa wanafunzi,kwani Kama kila mwalimu atasimama ipasavyo kwenye suala hilo basi maadili yatakuwa mazuri


Naye Mbunge wa Arusha Mjini,Mrisho Gambo alisema kuwa Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya walimu na maslahi yao hivyo basi wanatakiwa wajitume 


Alidai kuwa zawadi au motisha ambayo.na yeye ameipata katika hafla hiyo ambayo ni kiasi cha Milioni moja ielekezwe moja kwa moja kwenye choo cha walemavu katika shule ya sekondari Kaloleni.

This is received, thanks for your comments, will come back to you

Previous Post Next Post