
Waziri wa viwanda na
biashara ,Innocent Bashungwa akizungumza na waandishi wa habari jijini
Arusha katika mkutano wa Wafanyabiashara wa jumuiya ya Afrika Mashariki
unaofanyika jijini Arusha.

Mwanzilishi wa
kampuni ya Quickmarc ,Jiten Shah akizungumza na waandishi wa habari
katika maonyesho ya Wafanyabiashara wa jumuiya ya Afrika .

Afisa masoko mkuu wa
kampuni ya Motisun Group iliyopo jijijini Dar es Saalam,Erhard Mlyansi
watengenezaji wa bidhaa mbalimbali yakiwemo mabati ya kiboko ,
akizungumza na waandishi wa habari katika maonyesho ya Wafanyabiashara
wa jumuiya ya Afrika Mashariki yaliyoandaliwa na Baraza la
Wafanyabiashara wa jumuiya ya Afrika Mashariki.
………….
Happy Lazaro,Arusha.
Waziri wa Mambo ya
nje na ushirikiano wa kimataifa,Paramagamba Kabudi amezitaka nchi za
jumuiya ya Afrika mashariki kuwekeza katika sekta ya miundo mbinu ili
kuwa na nishati ya kutosha kwa ajili ya ujenzi wa viwanda .
Amesema hatua hiyo
itawezesha biashara kukua kwa nchi za jumuiya hiyo kiwemo kuongeza
sayansi ,Teknolojia na ubunifu kwa Vijana wenye ujuzi wa kufanyakazi
kwenye viwanda hivyo.
Ameyasema hayo katika
mkutano wa Wafanyabiashara zaidi ya 1000 wa nchi za Afrika mashariki
ulioandaliwa na Baraza la Wafanyabiashara wa nchi za Afrika Mashariki
(EABC) unaofanyika kwa siku mbili jijini Arusha na kwenda sambamba na
maadhimisho ya miaka 20 ya jumuiya ya Afrika Mashariki.
Prof.Kabudi amesema
kuwa,nchi zilizo nyuma katika maendeleo ya viwanda zinapaswa kusaidiwa
ili kupata viwanda na kuweza kuzalisha bidhaa na kuuza kwenye soko la
pamoja la jumuiya ya Afrika Mashariki.
“lazima nchi ziwe na
viwanda vya kutosha na kufanyabiashara nzuri ,kwa sababu jumuiya ni ya
watu wote na lazima iwanufaishe wananchi wote”Amesema
Naye waziri wa
viwanda na biashara Innocent Bashungwa amesema kuwa uchumi wa nchi za
jumuiya ya Afrika Mashariki lazima ujengwe kupitia sekta binafsi za
viwanda,kilimo, Mifugo na kuimarisha miundo mbinu .
Amesema serikali ya
Tanzania inajitahidi kuweka mazingira Bora kwa wafanyabiashara ili
biashara zao zinakua na kuhakikisha wanafanyabiashara nje ya Tanzania
bila kikwazo chochote .
Waziri Bashingwa
ametumia wasaa huo kuwakaribisha wawekezaji kuja hapa nchini kuwekeza
viwanda kwa ajili ya vifungashio na kuviuza katika nchi wanachama.
Baadhi ya
Wafanyabiashara waliohudhuria mkutano huo, Erhard Mlyansi ambaye ni
Afisa masoko mkuu wa kampuni ya Motisun Group kutoka jijini Dar es
Saalamu inayotengeneza bidhaa mbalimbali za ujenzi na juisi ya Sayona
amelalamikia hatua ya kuigwa kwa bidhaa zao na kuuzwa katika nchi za
jumuiya ya Afrika mashariki jambo ambalo limekuwa likiwasababishia
usumbufu kibiashara .
Mwanzilishi wa
kampuni ya Quickmarc Jiten Shah alisema kuwa,wamekuwa wakifanya
biashara mbalimbali katika nchi za jumuiya kwa ushirikiano mkubwa
ambapo wamekuwa wakiendelea kupata mafanikio makubwa katika biashara
zao.