Katika tukio hilo mama yake Mueni
aliyetambulika kwa jina la Monica Matolo, 75, alipata majeraha kadhaa ya
moto na kukimbizwa hospitali ya rufaa ya Makueni kwa ajili ya matibabu.
Aidha, katika uokozi huo mali za thamani
zilishindwa kuokolewa na zikateketea. Taarifa zinaeleza kuwa nyumba
hiyo ilikuwa na harufu kali ya petroli jambo linaloonyesha kuwa kuna mtu
alihusika kuunguza nyumba hiyo.
Polisi wanamhisi kaka yake Mueni
kuhusika katika tukio hilo kutokana na kuwapo kwa mgogoro wa ardhi wa
kifamilia. Aidha, miili minne iliyokutwa katika tukio hilo ilibebwa na
kwenda kuhifadhiwa mochwari ya hospitali ya rufaa ya Makueni.