
Polepole ametoa kauli hiyo Leo Novemba 11, 2019 kupitia ukurasa wake wa Twitter, huku zoezi zima la uchaguzi huo likiwa limekumbwa na changamoto kadhaa ikiwemo wagombea wengi wa vyama mbalimbali kuenguliwa.
Kutokana na changamoto hizo, jana Waziri wa Nchi ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Selemani Jafo alitengua maamuzi yote na kuamua kuwaruhusu wagombea wote nchini waliochukua fomu na kuzirejesha kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa bila kujali kama walienguliwa isipokuwa kwa wale wasio raia wa Tanzania, hawakujiandikisha au wamejiandikisha mara mbili.
