DC ARUSHA ATOA MAAGIZO MAZITO KWA BARAZA LA MADIWANI

AWATAKA KUPITIA UPYA SHERIA ZA MAZINGIRA KUDHIBITI WACHAFUZI WA MAZINGIRA

Na Seif Mangwangi, Arusha

MKUU wa Wilaya ya Arusha, Joseph Mkude amelitaka Baraza la Madiwani la Jiji la Arusha kupitia upya Sheria ya mazingira pamoja na Sheria ndogo ndogo za Jiji hilo a kuona namna ya kuzikazia Ili kudhibiti watu wanaotupa taka hovyo.

Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Joseph Mkude akizungumza wakati wa zoezi la kufanya usafi katika hospitali ya Jiji la Arusha 

DC Mkude ametoa agizo hilo leo Januari3, 2025 wakati wa zoezi la kufanya usafi wa mazingira ya ndani na nje ya hospitali ya Jiji la Arusha iliyopo Njiro katika Kata ya Engutoto.

“ Kupitia zoezi hili napenda kutoa maelekezo kwa Baraza la Madiwani, nendeni mkapiitie upya Sheria za mazingira na kuona kama zina mapungufu Ili tuweze kuyarekebisha Ili kuweza kukabiliana vyema na waharibifu wa mazingira,” amesema.

Amesema kama kuna mahali Baraza hilo litakwama liwasiliane na ofisi yake Ili kukamilisha mchakato huo mapema na kwamba kama Kuna sheria itahitaji marekebisho ya Bunge na yenyewe ifanyiwe mchakato na kuwasilishwa bungeni.

DC Mkude amesema katika Jiji la Arusha bado Kuna watu wanaoendelea kutupa hovyo makopo na plastiki ngumu hivyo kunahitajika Sheria kali itakayowadhibiti.

Mratibu wa zoezi la usafi katika Kata za Engutoto, Sokoni one na Sombetini, Diwani wa viti maalum tarafa ya Elerai, Aminatha Salash Toure, amesema zoezi hilo lilizinduliwa Januari2, 2025 na Meya wa Jiji la Arusha Maximilian Iranghe katika zoezi la kufanya usafi katika soko la dampo ni endelevu.

Amesema Jiji limejipanga kufanya usafi maeneo mbalimbali ya umma na yenye mikusanyiko ya watu wengi lakini pia zoezi litafanyika hadi majumbani Ili kuhakikisha Jiji linakuwa safi maeneo yote.

“ Zoezi hili ni endelevu na tutafika hadi majumbani, niwaombe tu wananchi wenzangu tuunge mkono kampeni hii ambayo tumeipa jina la ng’arisha Jiji la Arusha, kwa kuwa ni kampeni inayotuhusu wote na sio watu fulani pekee, usafi ni jambo jema na Kwa kuwa huu ni mji wa utalii lazima tuwe namba Moja kwenye usafi,” amesema.


Afisa afya Jiji la Arusha, James Lebikoki amewataka wananchi wa Jiji hilo kuacha kutupa takataka hovyo kwa kuwa madhara yake ni makubwa kwa afya na miundo mbinu ya maji ikiwemo kuziba mito na mitaro inayotiririsha maji.

Amesema kutupa taka ngumu kama plastiki na makopo kipindi hiki kuna haribu miundo mbinu kama ya maji jambo ambalo halikubaliki “ tunaenda kukazia Sheria zetu Ili kudhibiti watu wakorofi wachache ambao hawataki kuelewa, wakishapigwa fainu kubwa wataacha tu wenyewe,” amesema.

This is received, thanks for your comments, will come back to you

Previous Post Next Post